SERIKALI YAWATAKA WANANCHI KUWAFICHUA WAHALIFU
Wananchi wametakiwa kushirikiana na Viongozi wa Serikali kuwafichua wamiliki wa Taasisi za Ukopeshaji fedha zisizo rasmi ili watakao bainika hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi, Bw. John Wanga, alipokutana na Timu ya wataalamu ya Wizara ya Fedha ambao wanaendelea kutoa elimu ya fedha kwa wananchi wa mkoa wa Kagera katika Wilaya nne za Bukoba, Missenyi, Muleba na Biharamulo.