SERIKALI KUANGALIA UPYA TOZO ZA STEMPU YA KIELEKTRONIKI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Fedha na Mipango inataka kuangalia upya tozo za Stempu za Kielektroniki (ETS) ambazo kwa miaka mitatu iliyopita sekta ya viwanda imekuwa ikilalamika kuwa tozo hizi zimekuwa kubwa.