RAS TANGA AHAKIKISHA UTAYARI WA WIKI YA FEDHA
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga (RAS), Bw. Rashid Mchatta, amewahakikishia wadau wa sekta ya fedha kuwa maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha yatakayofanyika jijini Tanga yatakuwa na mafanikio makubwa kutokana na maandalizi madhubuti na ushirikiano wa karibu kati ya Serikali na wadau husika.
Bw. Mchatta alitoa kauli hiyo ofisini kwake jijini Tanga wakati alipokutana na wataalamu kutoka Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, waliowasili mkoani humo kwa ajili ya maandalizi ya maadhimisho hayo yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Januari 19 hadi 26, 2026, katika Viwanja vya Usagara.
