POLISI WILAYANI MISSENYI WATAKIWA KUWA MABALOZI WA ELIMU YA FEDHA
Polisi Wilayani Missenyi wametakiwa kuwa mabalozi kwa wananchi wanaowazunguka ili kuwafikishia elimu ya masuala ya fedha waliyoipata kutoka kwa Timu ya Wataalamu ya Wizara ya Fedha iliyoko katika kampeni ya kutoa elimu ya fedha kwa umma katika mikoa mbalimbali nchini.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Polisi Wilaya ya Missenyi SP. Jonas Sira Soa, wakati akizungumza na Askari Polisi katika semina iliyofanyika katika Viwanja vya Kituo Cha Polisi Kyaka, Wilaya ya Missenyi, mkoani Kagera.