MKAGUZI MKUU WA NDANI KUONGEZA USIMAMIZI WA MAPATO NA MATUMIZI
Mkaguzi Mkuu wa Ndani (IAG), Bw. Benjamini Magai amesema ofisi yake itafanya mabadiliko makubwa katika taratibu za ukaguzi katika maeneo ya mapato na matumizi kutokana na mafunzo muhimu waliyoyapata katika Mkutano wa 10 wa Shirikisho la Taasisi za Wakaguzi wa Ndani Afrika (AFIIA)
Hayo aliyasema jijini Arusha wakati wa kuhitimisha siku tano za Mkutano wa 10 wa Shirikisho hilo uliowakutanisha zaidi ya wajumbe 1200 kutoka nchi 27 za Afrika na nje ya Afrika.