MHE. DKT. NCHEMBA ATETA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA AfG1-IM
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) amesema kuwa Tanzania imejipanga kukabiliana na mabadiliko ya sera za nje za Marekani kuhusu misaada kwa nchi za Afrika kwa kutumia rasilimali zake ndani kupitia Bajeti Kuu ya Serikali.
Mhe. Dkt. Nchemba amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Kwanza la Nchi za Afrika wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Adran Ubisse, kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya IMF na Benki ya Dunia, inayofanyika Jijini Washington D.C, nchini Marekani.