MADALALI WA MINADA WATAKIWA KUJISAJINI KIELEKTRONIKI.
Wizara ya Fedha imeandaa Mfumo wa Kielektroniki wa utoaji Leseni za Udalali na Uendeshaji minada ya hadhara unaowezesha uombaji na upatikanaji wa Leseni kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia simu za mkononi au kompyuta mpakato ili kuwaondolea wananchi adha na gharama ya kufuata leseni hizo jijini Dodoma.
Akizungumza wakati akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa katika Viwanja vya Nanenane, Jijini Dodoma, Msimamizi wa Mali za Serikali wizarani hapo, Bw. George Killo, alisema Mfumo huo utamuwezesha mwananchi kufanya usajili popote alipo hivyo kupata leseni yake kwa wakati.