KOICA YAONESHA NIA YA KUSAIDIA MFUKO WA AFYA ZANZIBAR
Tanzania pamoja na mambo mengine imeliomba Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) kusaidia Mfuko wa Afya wa Pamoja (Health Basket Fund) wa Serikali ya Mapinduzi-Zanzibar ili kuboresha huduma za Afya kwa wananchi kwa mwaka 2024/2025.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa KOICA anayesimamia nchi za Afrika Mashariki, Bw. Chon Gyong-shik, Seoul, Korea Kusini.