KATIBU MKUU -HAZINA AFANYA MAZUNGUMZO NA TIMU YA TMEA

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba, amekutana na kufanya mazungumzo na timu ya Taasisi ya TradeMark East Afrika (TMEA) leo jijini Dar es Salaam ambapo kulikuwa na utambulisho wa Afisa Mtendaji Mkuu mpya wa TMEA Bw. David Beer ambaye alianza kazi rasmi tarehe 01 mwezi Septemba 2022, na aliambatana na Afisa Mtendaji Mkuu aliyemaliza muda wake Bw. Frank Matsaert.