FURSA YA ELIMU YA FEDHA YAWAFIKIA WANANCHI SHINYANGA.
Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga mkoani Shinyanga, wamepata fursa ya kujifunza elimu ya fedha kuhusu uwekezaji, matumizi sahihi ya fedha binafsi, utunzaji wa fedha binafsi, mambo ya kuzingatia kabla ya kuchukua mikopo, faida ya kuwekeza kwa ajili ya maisha ya uzeeni na kustaafu ili kufanya maamuzi sahihi wanapotumia huduma za fedha na kukuza uchumi.
Akizungumza kuhusu maeneo yatakayofikiwa katika mkoa wa Shinyanga, Afisa Usimamizi wa Fedha kutoka Wizara ya Fedha, Idara ya Uendelezaji Sekta ya Fedha, Bi. Elizabeth Mnzava, aliwaomba wananchi kutoa ushirikiano kupata elimu ya fedha kutokana na umuhimu wa elimu hiyo katika kukuza uchumi wa wananchi na nchi kwa ujumla.