ELIMU YA FEDHA KUFUNGUA FURSA ZA UKUAJI WA UCHUMI
Serikali imekusudia kuhakikisha wananchi wengi wanapata uelewa wa masuala ya fedha ili kuwawezesha kunufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana katika huduma rasmi za fedha na kuongeza kasi ya ukuaji wa Uchumi.
Hayo yameelezwa jijini Dodoma na Kamishna wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, kutoka Wizara ya Fedha, Dkt. Charles Mwamwaja, wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Maadhimisho ya tatu ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa kwa mwaka 2023 yanayotarajiwa kufanyika jijini Arusha.