DKT. NCHEMBA AKUTANA NA UONGOZI WA KAMPUNI YA SINOSURE
Tanzania na Taasisi ya Bima ya SINOSURE ya China zimeingia makubaliano yatakayoiwezesha Tanzania kunufaika na huduma za taasisi hiyo inayotoa dhamana kwa Taasisi za Fedha za China kwa ajili ya kuwezesha utekelezaji wa miradi ya uchumi ya serikali na sekta binafsi.
Makubaliano hayo yamefikiwa Mjini Beijing-China, wakati wa ziara ya ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu, ambapo ujumbe huo, pamoja na mambo mengine, una lengo la kuimarisha uhusiano na Taasisi za Fedha za China ili kupata fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa nchini.