DKT NCHEMBA AHIMIZA MATUMIZI YA KISWAHILI MIKUTANO YA BENKI YA DUNIA NA IMF
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amerejea wito wa Tanzania kwa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kukifanya Kiswahili kuwa miongozi mwa lugha rasmi za mawasiliano katika mikutano ya Taasisi hizo kubwa za Fedha Duniani.
Dkt. Nchemba ametoa rai hiyo alipoongoza Ujumbe wa Tanzania katika mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwakwa, Jijini Washington D.C, nchini Marekani, ambako Mikutano ya Mwaka ya Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF na Benki ya Dunia inafanyika.