CHUO CHA IAA CHATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU
Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kimetakiwa kuongeza ubunifu katika utendaji kazi wake ili kuongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani yatakayowezesha Chuo hicho kujiendesha kikamilifu kwa kutumia mapato hayo.
Maagizo hayo yametolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Jenifa Omolo, wakati wa ziara yake katika Chuo hicho ambapo alitembelea miradi inayotekelezwa pamoja na kuzungumza na Menejimenti ya Chuo hicho, jijini Arusha.