CHANDE ASHAURI MABENKI KUTANUA WIGO WA MASOKO NJE YA NCHI
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), ameitaka Akiba Commercial Bank Plc (ACB) kuendelea na jitihada za kuongeza wigo wa uwekezaji na masoko nje ya nchi ili kujiimarisha.
Mhe. Chande ametoa rai hiyo alipokutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Akiba Commercial Bank Plc (ACB), Bw. Silvest Arumasi, kuhusu fursa za maendeleo, Ofisini kwake, jijini Dodoma.
Alisema kuwa Sekta ya Benki nchini ikikua, itatoa fursa kwa Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kupitia benki za ndani kuliko kulazimika kwenda kutafuta fedha kwenye benki za nje ambazo hazimnufaishi mwananchi kwa kiwango kikubwa.