BENKI YA DUNIA KUENDELEZA USHIRIKIANO NA TANZANIA
KATIBU Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Natu Mwamba, amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha uhusiano na ushirikiano wake na Benki ya Dunia ili kuharakisha maendeleo ya nchi kiuchumi na kijamii.
Dkt. Mwamba amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia anayesimamia, Kundi Namba Moja Afrika, Dkt. Zarau Kibwe, aliyefika Ofisi za Hazina, Jijini Dodoma, kujitambulisha.