AFRICA 50- AfDB KUSAIDIA UJENZI WA BANDARI SHIRIKISHI ZANZIBAR
Serikali ya Tanzania na Taasisi ya Uwekezaji wa Miundombinu Afrika (Africa 50) kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), wamekubaliana kuendeleza huduma za bandari Visiwani Zanzibar.
Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Zanzibar, Dkt. Juma Malik Akil kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, katika kikao kati ya Tanzania na Taasisi hiyo kilichofanyika kando ya Mikutano ya Mwaka 2024 ya Bodi ya Magavana (Mawaziri wa Fedha kutoka nchi wanachama) wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Jijini Nairobi nchini Kenya.