Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

WIZARA YA FEDHA YAKABIDHI KADI ZA BIMA YA AFYA KWA WANAFUNZI SHULE MAALUM BUIGIRI

17 Jan, 2024
WIZARA YA FEDHA YAKABIDHI KADI ZA BIMA YA AFYA KWA WANAFUNZI SHULE MAALUM BUIGIRI
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi.Jenifa Christian Omolo (wa kwanza kushoto) akimkabidhi Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Maaluum ya Wasioona Buigiri, Bw. Samwel Jonathan (wa kwanza kulia) kadi 100 za bima ya afya za Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo, mkoani Dodoma. Kulia kwake ni wawakilishi wa viongozi wa Chama cha Wafanyakazi TUGHE tawi la Wizara hiyo, Bi. Scholastica Okudo, Bi. Halima Juma, Bi. Mariam Kiangi na Afisa Elimu Kata ya Buigiri, Mwalimu Emmanuel Otta.
 
 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo, amekabidhi kadi 100 za Bima ya Afya za Mfuko wa Bima ya Taifa (NHIF) kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi Maalum ya Wasioona, Buigiri, iliyoko Wilayani Chamwino mkoani Dodoma.
 
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi kadi hizo iliyofanyika katika shule hiyo, Bi. Omolo alisema kadi hizo sehemu ya kutekeleza ahadi iliyotolewa na watumishi wanawake wa Wizara hiyo mwaka 2023.
 
“Sisi kama jamii ya watumishi wanawake wa Wizara ya Fedha, kwa niaba ya Katibu Mkuu wetu, Dkt. Natu El – maamry Mwamba, tumeleta Kadi hizi ili kuwarahishia matibabu watoto wetu, tunaamini hatua hii itarudisha tabasamu kwa watoto wetu ambao ni zawadi kutoka kwa Mungu na kuongeza ari ya kufanya vizuri zaidi katika masomo yao ili kufikia malengo wanayoyatarajia”, alisema Bi. Omolo.
 
Alisema kadi hizo zina vifurushi vya mwaka mmoja na kuahidi kuwa Wizara itaendelea kuwalipia vifurushi kila mwaka.
 
Alitoa wito kwa taasisi na watu binafsi nchini kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu ili kuwawezesha kutimiza ndoto zao.
 
Aidha, aliupongeza uongozi wa shule hiyo kwa kuendelea kuwalea watoto hao katika maadili mema.
 
Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Samwel Jonathan, aliishukuru kwa msaada huo muhimu kwa afya za Watoto na kuomba Wizara iendelee kuwakumbuka kila wakati.
 
Naye Mwanafunzi wa Shule hiyo, Stanley Keneth, aliishukuru Wizara kwa kuwapatia kadi hizo na kubainisha kuwa bima hizo zitawasaidia kupata matibabu watakapopata changamoto za kiafya..
 
Bi Lucy Assay, ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Chamwino, aliishukuru Wizara ya Fedha kwa msaada huo na kutoa rai kwa jamii kutowaficha Watoto wenye mahitaji maalumu majumbani ili wapate elimu kwa kuwa shule zipo kulingana na namna ya ulemavu.
 
‘‘Niwashukuru sana kwa msaada mliotoa kwa kuwa sasa watoto wetu wataweza kupata huduma za afya na nitoe rai kwa jamii kuwa na moyo wa kusaidia watu wenye mahitaji maalumu’’alisema Bi. Lucy.
 
Shule ya Msingi Buigiri ni ya pekee mkoani Dodoma inayotoa elimu ya makundi maalum na ilianzishwa Aprili 30, 1950, inafundisha Watoto wenye uoni hafifu, wasioona pamoja na wenye ulemavu wa ngozi kuanzia shule ya awali hadi darasa la saba.
 

MWISHO.