Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

WIZARA YA FEDHA YAANZA KUTOA ELIMU YA FEDHA KUPITIA SANAA

19 Jan, 2024
WIZARA YA FEDHA YAANZA KUTOA ELIMU YA FEDHA KUPITIA SANAA

Afisa Msimamizi wa Fedha Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro, akielezea umuhimu wa usajili wa vikundi vya kijamii vya huduma ndogo za fedha, wakati wa kutoa elimu ya fedha kwa vitendo kwa njia ya sanaa katika Mtaa wa Malikula Chamwino mkoani Morogoro.

 

Wizara ya Fedha kupitia Shirika la Kijamii linalojishughulisha na utoaji Elimu ya Uraia (TACCI) wamefanikiwa kuwafikishia elimu ya Fedha baadhi ya wakazi wa Morogoro kwa njia ya Sanaa ikiwa ni mwanzo wa mkakati wa kufikisha elimu hiyo nchi zima ili kutekeleza Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha kwa kwaka 2021/2022 hadi 2029/2030.

Akizungumza baada ya elimu hiyo iliyotolewa mtaa wa Malikula Chamwino, mkoani Morogoro, Afisa Msimamizi wa Fedha Mkuu kutoka Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro, alisema kuwa elimu kwa njia ya Sanaa mkoani Morogoro ni mwanzo wa matukio kama hayo yatakayofanyika nchi nzima hususan maeneo ya vijijini kwa kuwa njia hiyo imeonesha mafanikio makubwa.

“Lengo kubwa ni kufika vijijini ambako kuna uelewa mdogo wa masuala ya elimu ya Fedha na tutajitahidi kuchagua maeneo mahususi ambayo yameainishwa kwenye utafiti wa FISCOPE wa mwaka 2023 ambao unaonesha ujumuishwaji mdogo wa masuala ya fedha unaochangiwa na uelewa mdogo”, alieleza Bw. Kimaro.

Kwa upande wake Mtaalamu wa masuala ya Vikundi vya Kijamii vinavyotoa Huduma Ndogo za Fedha, Bw. Joseph Msumule, alisema kuwa muitikio wa wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza elimu ya fedha kumechangiwa na Sanaa ya maigizo na ngoma iliyofanywa kwa weledi mkubwa ikilenga elimu ya fedha kwa njia rahisi.

Alisema maigizo hayo yalilenga kuweka akiba, uwekezaji, mifuko ya hifadhi ya jamii, usimamizi binafsi wa masuala ya fedha na namna ya kusajili vikundi ili kuepusha wananchi kudhulumiwa na kukopa maeneo ambayo hayajaainishwa katika Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha.

Kwa upande wao wananchi wa mtaa wa Chamwino Morogoro, wameipongeza Wizara kwa kuwapelekea elimu ya fedha kwa njia ya sanaa kwa kuwa inawarahisishia kuelewa na wapo tayari kuanza kuifanyia kazi kwa kuwashinikiza viongozi wa vikundi vya Kijamii vya Huduma ndogo za Fedha (CMG) kujisajili kwa mujibu wa Sheria.

Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha unalengo la kuhakikisha hadi kufikia mwaka 2025 asilimia 80 ya wananchi wawe na uelewa wa kutosha wa elimu ya fedha.

Mwisho.