Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

WADAU WAALIKWA KUTOA MAONI YA KODI KUPITIA MFUMO WA KIELEKTRONIKI

23 Jun, 2025
WADAU WAALIKWA KUTOA MAONI YA KODI KUPITIA MFUMO WA KIELEKTRONIKI

Afisa Usimamizi wa Fedha Mwandamizi, Idara wa Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Bw. Daved Massawe akitoa elimu kwa Bi. Zainabu Kyama kuhusu huduma zinazotolewa katika Banda la Wizara ya Fedha, kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma. 

 

Wizara ya Fedha imetoa wito kwa wananchi kujenga mazoea ya kushiriki mchakato wa kutoa maoni ya maboresho ya mfumo wa kodi kupitia mfumo wa kieletroniki wa kuwasilisha maoni (Maoni Portal) ili Serikali iweze kuyafanyia kazi kwa maendeleo ya uchumi wa nchi.

Wito huo umetolewa na Afisa Usimamizi wa Fedha Mwandamizi, Idara ya Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Bw. David Massawe, wakati akitoa elimu ya masuala ya kodi kwa watu waliotembelea Banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma.

“Mwezi Desemba kila mwaka, Serikali kupitia Wizara ya Fedha hutoa fursa kwa wananchi kupitia dirisha la mfumo wa kieletroniki wa maoni portal ambapo wananchi hualikwa kuwasilisha maoni ya kuboresha mfumo wa kodi ili kuhakikisha kuwa sera za kodi nchini zinazingatia kanuni za usawa, ufanisi, kuakisi matakwa ya wananchi na zenye kuendana na mazingira halisi ya kiuchumi nchini” alisema Bw. Massawe.

Aliongeza kuwa makundi mbalimbali yakiwemo taasisi binafsi na taasisi za umma, wakiwemo wafanyabiashara, wakulima, vijana, wanawake na wastaafu wanashiriki kutoa maoni ili Serikali iweze kuandaa sera za kodi rafiki kwa makundi yote.

Wiki ya Maadhimisho ya Utumishi wa Umma imeanza Juni 16 na inatarajiwa kuhitimishwa Juni 23 mwaka huu ikiwa na kauli mbiu ya “Himiza Matumizi ya Mifumo ya Kidigiti ili kuongeza Upatikanaji wa Taarifa na Kuchangia Uwajibikaji”.

MWISHO.