Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

TANZANIA KUTUMIA FURSA ZA UWEKEZAJI KUTOKA BENKI YA AFREXIM

19 Jul, 2022
TANZANIA KUTUMIA FURSA ZA UWEKEZAJI KUTOKA BENKI YA AFREXIM

Na. Peter Haule, WFM, Dodoma

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba amemuahidi Rais wa Benki ya Afrexim kuongeza mtaji wa ziada katika Benki hiyo ambayo Tanzania inamiliki hisa ili iwe na wigo mpana wa kuendelea kupata rasilimali fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

Dkt. Nchemba ametoa ahadi hiyo jijini Dodoma alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Benki ya Afrexim, Prof. Benedict Oramah, ambapo walijadili masuala kadhaa likiwemo  fursa zinazotolewa na Benki hiyo.

Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali itashirikiana na Benki hiyo ambayo kuanzishwa kwake kulikuwa na lengo la kusaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika nchi za Afrika.

“Tunatekeleza dira ya Mhe. Rais ya kuweza kuvutia uwekezaji, kuendeleza maeneo mahususi ya uwekezaji (EPZ) pamoja na upande wa Zanzibar ambayo inakusudiwa kutengeneza ajira nyingi kwa vijana ili pato la mtanzania mmojammoja liongezeke na kuweza kupunguza umasikini”, alieleza Dkt. Nchemba.

Aidha Dkt. Nchemba amesema kuwa Tanzania inaahidi kuendelea kufanyakazi pamoja na ofisi ya Rais huyo kwa kuzishirikisha Wizara zake, ikiwemo ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Wizara ya Kilimo na Afya ili kuweza kutumia fursa zilizobainishwa na Benki hiyo.

Kwa upande wake Rais wa Benki ya Afrexim, Prof. Benedict Oramah, alisema kuwa Benki yake inafursa nyingi zikiwemo za mikopo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya barabara, afya na viwanda.

Alizitaja fursa nyingine ambazo Tanzania inaweza kuzipata kuwa ni pamoja na  kuwezesha Kanda maalum za kiuchumi, kuongeza thamani ya mazao ya kilimo pamoja na uwekezaji katika hisa kupitia taasisi za fedha.

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) akizungumza jambo wakati wa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kulia) na Rais wa Benki ya Afrexim, Prof. Benedict Oramah (hayupo pichani), jijini Dodoma.

Mwisho.