Category Title
-
01 Mar, 2022The Microfinance (Saving and Credit Cooperative Societies) Regulations, 2019
-
01 Mar, 2022The Microfinance (Non- Deposit Taking Microfinance Service Providers) Regulations, 2019
-
28 Feb, 2022The Microfinance (Community Microfinance Groups) Regulations, 2019
-
View All
-
28 Feb, 2022MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA 2022/23
-
28 Feb, 2022MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA 2021/22
-
05 Nov, 2021Budget Guideline 2008 - 09 Part II
-
05 Nov, 2021Budget Guideline 2008 - 09 Part I
-
05 Nov, 2021Budget Guideline 2009 - 10 Part II
-
05 Nov, 2021Budget Guideline 2011 -12
-
05 Nov, 2021Budget Guideline 2013 - 14
-
05 Nov, 2021Annexes to the Guidelines for 2013 - 14
-
05 Nov, 2021Budget Guideline 2014 - 15
-
05 Nov, 2021Annexes to the Guidelines 2014 -15
-
View All
-
02 Mar, 2022Implementation Strategy for the National Development Plan 2016/17 – 2020/21 Volume IV - Communication strategy April, 2018.
-
01 Mar, 2022Implementation Strategy for the National Five - Year Development Plan 2016/17 – 2020/21 VOLUME II
-
28 Feb, 2022M&E Strategy of the 2nd FYDP
-
27 Feb, 2022The Action Plan of Implementation of the 2nd FYDP
-
View All
-
30 Apr, 2022THE BUDGET EXECUTION REPORT FOR THE SECOND QUARTER OF 2021/22
-
29 Apr, 2022BER Q1 2021- 22-FINAL
-
02 Mar, 2022THE BUDGET EXECUTION REPORT 2020/21 (JULY 2020 TO JUNE 2021)
-
01 Mar, 2022Budget Execution Report (BER) for the First Quarter of 2020-21
-
01 Mar, 2022The Budget Execution Report for the Second Quarter of 2020/21
-
01 Mar, 2022The Budget Execution Report for the Third Quarter of 2020/21
-
28 Feb, 2022THE BUDGET EXECUTION REPORT FOR THE THIRD QUARTER OF 2018/19 (JANUARY – MARCH, 2019)
-
View All
-
03 Mar, 2022GOVERNMENT BUDGET CITIZENS’ EDITION 2021/2022
-
02 Mar, 2022GOVERNMENT BUDGET CITIZENS’ EDITION 2020/2021
-
01 Mar, 2022GOVERNMENT BUDGET CITIZENS’ EDITION 2019/2020
-
28 Feb, 2022GOVERNMENT BUDGET CITIZENS’ EDITION 2018/2019
-
25 Feb, 2022GOVERNMENT BUDGET CITIZENS’ EDITION 2017/2018
-
20 Feb, 2022GOVERNMENT BUDGET CITIZENS’ EDITION 2016/2017
-
View All
-
Budget Books 2021/2022
-
Budget Books 2020
-
Budget Books 2018/2019
-
Budget Books 2015/2016
-
Budget Books 2014/2015
-
Economic Survey Books
-
07 Mar, 2022VOLUME II ESTIMATES OF PUBLIC EXPENDITURES AS PASSED BY THE PARLIAMENT 2021.2022 (MINISTERIAL)
-
06 Mar, 2022VOLUME III ESTIMATES OF PUBLIC EXPENDITURES AS PASSED BY THE PARLIAMENT 2021.2022 (REGIONAL)
-
05 Mar, 2022VOLUME IV PUBLIC EXPENDITURE ESTIMATES DEVELOPMENT VOTES AS PASSED BY THE PARLIAMENT 2021.2022 (Ministerial and Regional Development Programmes)
-
04 Mar, 2022VOLUME I Financial Statement & Revenue Estimates for the year from 1 July 2021- to 30th June 2022
-
03 Mar, 2022VOLUME II Estimates of Public Expenditure Consolidated Fund Services and Supply Votes (Ministerial) - 2021.22
-
28 Feb, 2022VOLUME III Estimates of Public Expenditure Supply Votes (Regional) - 2021-22
-
27 Feb, 2022VOLUME IV Public Expenditure Estimates Development Votes (Ministerial and Regional Development Programmes ) - 2021.22
-
View All
- Content not found
-
03 Mar, 2022VOLUME I - FINANCIAL STATEMENT AND REVENUE ESTIMATES 2018-19
-
02 Mar, 2022volome II 2018_19
-
28 Feb, 2022Volume III 2018_19
-
27 Feb, 2022volome IV 2018_19
-
26 Feb, 2022KITABU CHA MKAKATI WA KUZIWEZESHA HALMASHAURI KUJITEGEMEA KIMAPATO
-
View All
-
03 Mar, 2022Volume II -as passed 2014-15
-
02 Mar, 2022Volume III -as passed 2014-15
-
01 Mar, 2022volume IV-as passed 2014-15
-
View All
-
02 Mar, 2022Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2021.22
-
28 Feb, 2022KITABU CHA HALI YA UCHUMI WA TAIFA KATIKA MWAKA 2018
-
27 Feb, 2022KITABU CHA HALI YA UCHUMI WA TAIFA KWA MWAKA 2017
-
View All
- Content not found
- Content not found
-
03 Mar, 2022Audited Consolidated Financial Statements for the year ended 30th June, 2020"
-
02 Mar, 2022Audited Consolidated Financial Statements for the year ended 30th June, 2019"
-
28 Feb, 2022Audited Consolidated Financial Statements for year ended 30th June, 2018
-
27 Feb, 2022Audited Consolidated Financial Statements for year ended 30th June, 2017
-
View All
TAASISI ZA UMMA ZAAGIZWA KUTUMIA MFUMO WA TANePS

TAARIFA KWA UMMA
TAASISI ZA UMMA ZAAGIZWA KUTUMIA MFUMO WA TANePS
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha kuwa taasisi zote za umma zinatumia Mfumo wa Ununuzi kwa Njia ya Mtandao (TANePS) na hatua kali zichukuliwe dhidi ya maafisa masuuli ambao taasisi zao zitakaidi matumizi ya mifumo katika ununuzi wa umma.
Maagizo hayo aliyatoa jijini Arusha, wakati akifungua kongamano la Wiki ya ununuzi wa Umma lililowakutanisha wadau wa ununuzi takribani 1000 wakiwemo maafisa ugavi, wazabuni, wajumbe wa bodi na maafisa masuuli kutoka Wizara, taasisi, Halmashauri na sekta binafsi.
Akizungumza katika kongamano hilo Mhe. Majaliwa alisisitiza matumizi ya mifumo katika ununuzi wa umma pamoja na kuhakikisha ufanisi wa mifumo hiyo ili huduma zipatikane kwa wakati ukiwemo umakini wa wanaosimamia mifumo na kuwa na njia mbadala ikitokea changamoto ya mtandao.
‘Wizara ya Fedha na Mipango ifanye tathmini na maboresho ya mifumo na taratibu za ununuzi ili kudhibiti mianya iliyopo inayosababisha Serikali kupoteza fedha nyingi kwa huduma ambazo kiuhalisia bei zake ni za chini,’ alisema Mhe. Majaliwa.
Alisisitiza kuwa ili kupata thamani halisi ya fedha katika ununuzi wa umma usimamizi madhubuti unahitajika katika sekta hiyo hasa kwa kuzingatia kuwa zaidi ya asilimia 70 ya Bajeti ya Serikali ambayo inatokana na fedha za walipa kodi, inatumika katika ununuzi wa bidhaa, huduma na kandarasi za ujenzi.
Alisema kuwa kipindi kinachoishia Machi 2022 jumla ya zabuni 48,487 zenye thamani ya Sh. trilioni 22.7 zimechakatwa, hivyo fedha hizo zinazotumika kwenye ununuzi zinahitaji usimamizi madhubuti kwa kuwa kinahusisha matumizi ya fedha za walipa kodi.
Pia Mhe. Majaliwa aliiagiza Wizara ya Fedha na Mipango kupitia kitengo chake cha Usimamizi wa Mifumo ya Taarifa za Kifedha na GPSA ihakikishe bei zote za bidhaa na huduma zinazotumika sokoni kwa jumla na rejareja zinaingizwa kwenye mfumo wa TANEPS na kuwa na kiwango cha ukomo wa bei zitakazotumika Serikalini.
Aidha amewataka wadau wa kongamano la Wiki ya ununuzi wa umma kutumia wiki hiyo kuendelea kuhamasishana, kupeana uzoefu na pia kujadiliana namna bora zaidi ya kuendelea kutumia teknolojia kuboresha ununuzi wa umma nchini, pamoja na kuelimisha wananchi umuhimu wa teknolojia katika manunuzi ya umma.
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), katika kongamano hilo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb) alisema Serikali imechukua hatua mbalimbali katika kuboresha sekta ya ununuzi wa umma kwa maslahi ya Taifa kwa kufanya maboresho katika Sheria ya ununuzi wa umma.
Alisema maboresho hayo ni pamoja na kurekebisha vifungu vilivyokuwa vinakwamisha utekelezaji wa ununuzi kwa ufanisi na kuhakikisha kuwa sekta ya ununuzi inawashirikisha watanzania wa makundi yote katika kujenga uchumi wa Taifa.
‘Faida zilizotokana na marekebisho ya Sheria ni pamoja na kupungua kwa muda wa mchakato wa ununuzi, ushughulikiaji wa malalamiko ya wazabuni, upendeleo kwa makampuni yanayomilikiwa na watanzania na upendeleo kwa makundi maalumu ya vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu’ alisema Mhe. Chande.
Alisema kuwa Serikali imeendelea na jitihada za kuimarisha utekelezaji wa ununuzi wa umma nchini kwa kuanzisha na kusimamia utekelezaji wa mifumo ya kielektroniki katika kudhibiti matumizi na kuongeza ufanisi kwenye ununuzi wa umma.
Aidha, Mhe. Chande alieleza kuwa wiki ya ununuzi wa umma inatoa fursa kwa wadau wa ununuzi wa umma na ugavi kubadilishana uzoefu pamoja kufanya maonesho ya huduma wanazotoa kwa jamii.
Kongamano la Wiki ya ununuzi wa Umma limeandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango na taasisi zinazosimamia ununuzi wa umma nchini ambazo ni Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA), Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA), Mamlaka ya Rufaa za Zabuni za Umma (PPAA) na Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB).
Imetolewa na:
Benny Mwaipaja
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha ya Mipango