Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

SERIKALI: BIMA NI BIASHARA HURIA

17 May, 2022
SERIKALI: BIMA NI BIASHARA HURIA

TAARIFA KWA UMMA

 

Serikali imesema biashara ya bima nchini ni huria inayoendeshwa na kampuni za bima zipatazo thelathini na moja ikiwemo Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC) ambapo kwa mujibu wa Sheria ya Bima namba 10 ya mwaka 2009, kampuni yoyote ya Bima, iliyosajiliwa, ina haki ya kuweka kinga ya bima kwenye miradi mikubwa.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Kundo Methew (Mb) kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Gando Mheshimiwa Mussa Omar Salim, aliyetaka kujua kama kuna mwongozo wowote unaoeleza kuwa Shirika la Bima la Zanzibar haliruhusiwi kushiriki kukata bima za miradi mikubwa.

“Shirika la Bima la Zanzibar (Zanzibar Insurance Corporation- ZIC) limesajiliwa na kupewa leseni ya biashara namba 00000821 na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania –TIRA, chini ya Sheria ya Bima Na. 10 ya mwaka 2009. ZIC inafanya biashara za bima sehemu zote Tanzania Bara na Zanzibar.” Alisema Mhe. Kundo

Mheshimiwa Kundo alisema kuwa Hakuna mwongozo wowote unaokataza Zanzibar Insurance Corporation (ZIC) kushiriki katika biashara ya kukata bima za miradi mikubwa nchini.

Imetolewa na:

Benny Mwaipaja

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Wizara ya Fedha ya Mipango