Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

NORWAY KUKIJENGEA UWEZO KITUO CHA UBIA KATI YA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI

02 Feb, 2024
NORWAY KUKIJENGEA UWEZO KITUO CHA UBIA KATI YA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) (kulia), akisalimiana na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Tone Tinnes, walipokutana ofisini kwakwe jijini Dodoma kwa ajili ya kufanya mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na nchi hiyo.

 

Norway imeonesha nia ya kushirikiana na Tanzania katika kukijengea uwezo Kituo cha Ubia kati ya Serikali na Sekta binafsi ili kuiwezesha sekta binafsi kushiriki kikamilifu kujenga Uchumi wa nchi.

Hayo yameelezwa jijini Dodoma, na Mhe. Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Tone Tinnes, kuhusu ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Dkt. Nchemba alisema kuwa kiu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ni kuona kuona sekta binafsi inashiriki katika kujenga Uchumi wa nchi, kutengeneza ajira kwa wananchi wakiwemo vijana na wanawake na kutengeneza vyanzo vipya vya kodi.

Aidha, Dkt. Nchemba alieleza kuwa, Norway imepiga hatua kubwa katika eneo la kodi na kuishauri nchi hiyo iangalie namna ya kushirikiana na Tanzania katika kubadilishana ujuzi katika eneo hilo na masuala mengine ya kifedha

Akizungumzia kuhusu mabadiliko ya Tabianchi, Mhe. Dkt. Nchemba alisema kuwa eneo hilo ni muhimu kwa Tanzania, ambapo ameiomba Norway ambayo imepiga hatua katika eneo hilo, kushirikiana na Tanzania ili iweze kupata vigezo muhimu vya kupatiwa fedha kwa ajili ya kukabiliana na changamoto ya mabadiliko hayo.

Dkt. Nchemba ameishukuru Norway kwa mchango wake katika maendeleo ya nchi katika sekta mbalimbali ikiwemo miundombinu, nishati, elimu, kilimo na ustawi wa jamii.

Kwa upande wake Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Tone Tinnes, alisema kuwa Ushirikiano wa nchi hizo mbili umetimiza zaidi ya miaka 60, na katika kipindi hicho nchi yake imeshiriki katika maendeleo kwenye Sekta za miundombinu, nishati, kilimo, na pia imeshiriki katika uanzishwaji wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) na imechangia kujenga mitambo ya umeme wa maji.

Alisema kuwa katika eneo la Kilimo, nchi yake inaadhimisha miaka 50 ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) kwa kutoa ujuzi na pia imekuwa na mchango wa ujuzi katika taasisi mbalimbali ikiwemo Wizara ya Fedha.

Mhe. Tone Tinnes, ameipongeza Tanzania kwa kupiga hatua kubwa ya maendeleo na kuahidi kuwa nchi yake iko tayari kutoa kutoa ushirikiano katika kufanikisha mahitaji mapya ili kuharakisha maendeleo zaidi.

Alilitaja eneo mahususi ambalo nchi yake itashirikiana na Tanzania ni kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi jambo ambalo limekuwa na changamoto si tu kwa Tanzania nali pia Dunia nzima kwa ujumla, na kusisitiza kuwa kilimo kinatakiwa kutekelezwa kwa kuangalia athari ya mabadiliko ya Tabia nchi.

Mwisho.