Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

HALI YA UPATIKANAJI WA CHAKULA NCHINI YASAIDIA KUPUNGUZA UMASIKINI

14 Nov, 2023
HALI YA UPATIKANAJI WA CHAKULA NCHINI YASAIDIA KUPUNGUZA UMASIKINI
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), akifungua Mkutano wa Maadhimisho ya Miaka 15 ya Mradi wa Utafiti wa Kupima Hali ya Maisha zinazojumuisha Tafiti za Kilimo Katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, uliofanyika katika Hoteli ya Delta jijini Dar es salaam. Mkutano huo wa siku mbili umehudhuriwa na watalamu wa uchumi, sera na watafiti kutoka nchi mbalimbali za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo matokeo ya baadhi ya tafiti zilizofanyika chini ya mradi huo zinawasilishwa.  
 
 
Tanzania imekuwa kwenye kiwango kizuri cha upatikanaji wa chakula kutokana na kuwepo kwa takwimu sahihi za hali ya Maisha katika kaya, hali iliyopolekea kiwango cha umasikini wa chakula kushuka nchini.
 
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), wakati akifungua Mkutano wa Maadhimisho ya Miaka 15 ya Mradi wa Utafiti wa Kupima Hali ya Maisha zinazojumuisha Tafiti za Kilimo Katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (Living Standards Measurement Study-Intergrated Survey on Agriculture (LSMS-ISA), katika Hoteli ya Delta, jijini Dar es Salaam.
 
Amesema Programu hiyo ya utafiti iliyoanza 2008 ambayo ilifadhiliwa na Benki ya Dunia imeweka alama sio tu katika uzalishaji wa takwimu muhimu za hali ya maisha katika kaya bali pia takwimu zilizozalishwa zimekuwa nyenzo muhimu za kutathmini sera na programu zinazotekelezwa na Serikali, taasisi binafsi na wadau wa maendeleo.
 
“Kiwango cha umasikini kwa sasa kimepungua hasa umasikini wa upatikanaji wa chakula, chakula kipo kwa wingi cha kutosha ambapo sisi watanzania leo tunalisha mpaka nchi jirani” amesema Chande
 
Kwa upande wake Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt Albina Chuwa, amesema miaka 15 ya mradi huo umeleta mafanikio makubwa nchini na barani Afrika kwa ujumla.
 
“Wakati utafiti unaanza 2008 katika Bara la Afrika nchi nyingi zilikua zinafanya utafiti kwa kutumia karatasi lakini sasa teknolojia imekuwa na sasa utafiti unafanywa kwa kutumia vishkwambi” amesema Dkt. Chuwa.
 
Naye, Meneja Miradi kutoka Benki ya Dunia, Bw. Gero Carletto, ameipongeza Tanzania kwa kuendelea kutoa ushirikiano katika programu hiyo na juhudi zinazochukuliwa na Serikali katika kupunguza umasikini wa chakula.
 
“ Kumekuwa na maendeleo makubwa sio tu katika kupunguza umaskini bali pia katika viashiria vingine vingi. Jopo la kitaifa la utafiti, limekuwa makini katika kuelewa vyema mienendo ya umaskini”. Bw. Carletto
 
Naye, Kamisaa wa Sensa, Mhe. Anna Makinda, amewataka watafiti kurudisha tafiti hizo kwa wananchi kwa maana wao ndio wahusika wakuu. Amesema utafiti huu umefanikiwa kwa sababu umeweza kumfikia mtu mmoja mmoja na kuelezea ukweli kuhusu maisha yake jambo ambalo si rahisi.
 
“Hawa wataalam wa takwimu tunasema sasa wakati umefika utafiti wao uenze kuwatumikia hawa wananchi lakini pia utasaidia utendaji wa serikali katika kuwahudumia wananchi wake” amesema Makinda.
 
Mkutano huo wa siku mbili umehudhuriwa na watalamu wa uchumi, sera na watafiti kutoka nchi mbalimbali za Kusini mwa Jangwa la Sahara ambapo matokeo ya baadhi ya tafiti zilizofanyika chini ya mradi huo zinawasilishwa.  
 
MWISHO