Category Title

  • Government Budget Speeches
  • Ministry's Budget Speeches
  • Budget Books 2024/2025
  • Budget Books 2023/2024
  • Budget Books 2022/2023
  • Budget Books 2021/2022
  • Budget Books 2020
  • Budget Books 2018/2019
  • Budget Books 2015/2016
  • Budget Books 2014/2015
  • Content not found
  • Content not found
  • Content not found

DKT. NATU MWAMBA ATETA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA MFUKO WA CIF, JIJINI WASHINGTON MAREKANI

27 Apr, 2025
DKT. NATU MWAMBA ATETA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA MFUKO WA CIF, JIJINI WASHINGTON MAREKANI

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba (Kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Uwekezaji katika Mabadiliko ya Tabianchi (Climate Investment Funds (CIF), Bi. Tariye Gbadegesin, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe, ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia ya mwaka 2025, inayofanyika jijini Washington D.C nchini Marekani, ambapo wamejadiliana masuala kadhaa kuhusu jinsi Mfuko wa CIF unavyoweza kusaidia juhudi za Tanzania katika kutekeleza Mpango wa Nishati (Energy Compact) na kuendeleza vipaumbele vya matumizi ya Nishati safi.

 

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Uwekezaji katika Mabadiliko ya Tabianchi (Climate Investment Funds (CIF), Bi. Tariye Gbadegesin, Kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe, ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia ya mwaka 2025, inayofanyika jijini Washington D.C nchini Marekani.
 
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani, Jijini Washington, Dkt. Mwamba na mgeni wake, wamejadiliana masuala kadhaa kuhusu jinsi Mfuko wa CIF unavyoweza kusaidia juhudi za Tanzania katika kutekeleza Mpango wa Nishati (Energy Compact) na kuendeleza vipaumbele vya matumizi ya Nishati safi.
 
MWISHO