Tanzania imejipanga kikamilifu kuwa kitovu cha uwekezaji barani Afrika na inawakaribisha wawekezaji wa Marekani kuchangamkia fursa lukuki zilizopo katika sekta mbalimbali za uchumi.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) wakati alipoongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Uwekezaji ulioandaliwa na Baraza la Biashara la Kimataifa- Business Council for International Understanding (BCIU), uliofanyika katika Ofisi za BCIU, jijini Washington D.C nchini Marekani, pembezoni mwa Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, ameshiriki katika hafla ya kifungua kinywa iliyowakutanisha wanawake viongozi kutoka sekta mbalimbali, iliyoandaliwa na Benki ya Dunia kupitia Wakurugenzi Watendaji wake, Bi. Anna Bjerde na Bi. Anshula Kant, katika Ofisi za Benki hiyo jijini Washington D.C nchini Marekani, kando ya Mikutano ya Majira ya Kipupwe ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa-IMF inayoendelea jijini humo.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, ameishauri Benki ya Dunia kuangalia namna ya kuiwezesha sekta binafsi katika nchi za Afrika ili iweze kuwa imara na kuchangia kukuza uchumi wa nchi hizo.
Mhe. Balozi Omar, ametoa wito huo wakati akichangia mada katika mkutano wa Kundi la Kwanza la nchi za Kanda ya Afrika, wanachama wa Benki ya Dunia (Africa Group 1 Constituency), uliofanyika Makao Makuu ya Benki hiyo, Jijini Washington D.C, nchini Marekani.
Tanzania imeendelea kuimarisha ushirikiano wake na Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu ya Asia (AIIB), hatua inayotarajiwa kufungua fursa mpya za ufadhili kwa miradi ya kimkakati ya maendeleo, ikiwemo maji, nishati, usafiri, teknolojia ya habari na Mawasiliano pamoja na miundombinu ya kijani.
Meza Kuu ikiongozwa na Mgeni Rasmi Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), wakionesha Vitabu vya Sera Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025 na Mkakati Wa Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025 kwa Kipindi Cha Mwaka 2026–2036, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Sera hiyo katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma.
Serikali ya Tanzania imerejea tena dhamira yake ya kushirikiana kwa karibu na Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC) ili kuongeza uwekezaji wa sekta binafsi, kupanua miundombinu na kuharakisha Mpango wa Taifa wa mabadiliko ya nishati chini ya Dira ya Taifa ya Maendeleo (DIRA 2050).
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) ametoa rai kwa Taasisi ya Bima ya Maendeleo ya Biashara na Uwekezaji Afrika (ATIDI) kushirikiana na Tanzania hususani katika kukuza Sekta binafsi ili nchi iweze kufikia malengo ya Dira ya Taifa 2050.
Serikali kupitia Wizara ya Fedha imeendelea kung’ara kimataifa baada ya kushinda tuzo ya “Infrastructure Finance Deal of the Year 2026” zinazotolewa na Global Banking & Markets, kufuatia mafanikio ya upatikanaji wa mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani bilioni 1.78 kwa ajili kugharamia ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme (SGR) kwa kipande cha tatu na cha nne.
Serikali ya Tanzania imewakaribisha wawekezaji kutoka Uturuki kuwekeza katika sekta za kimkakati zikiwemo miundombinu, nishati na kilimo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuharakisha maendeleo ya uchumi na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
UZINDUZI WA SERA YA TAIFA YA USIMAMIZI WA MNYORORO WA UGAVI YA MWAKA 2025