Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza wakati wa akishiriki mjadala kuhusu nafasi ya sekta ya viwanda inavyoweza kuchangia ukuaji wa uchumi katika nchi Afrika, mjadala uliofanyika pembezoni mwa Mkutano wa African Caucus wa Mwaka 2026, unaofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha SDKJ, Banjul nchini Gambia, ambapo amesema kuwa nchi za Afrika zinahitaji kuchukua hatua madhubiti za kisera na kikodi ili kuiwezesha sekta ya viwanda kuchangia ukuaji wa uchumi, kukuza ajira, kuimarisha uzalishaji na kupanua mauzo ya nje.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb)(katikati), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Fedha wanaoshiriki katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwl. J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam, wakati alipotembelea banda la wizara hiyo.
Picha ya pamoja ya ujumbe wa Tanzania mara baada ya kumalizika kwa mijadala ya Mawaziri wa Fedha na Afya wa SADC uliofanyika Harare, Zimbabwe.
Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati), Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (wa tatu kulia), Mkurugenzi Mpya wa Benki ya Afrexim Kanda ya Afrika Mashariki, Bw. Humphrey Nwugo (wa tatu kushoto), na maafisa wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha na Benki ya Afrexim, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), pamoja na viongozi mbalimbali wa Mamlaka ya Mapato Tanzania wakiongozwa na Kamishna Mkuu wa TRA, Bw. Yusuph Juma Mwenda pamoja na wananchi wakimshuhudia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila, akizindua rasmi mbio na matembezi ya shukrani kwa walipakodi kuelekea Tuzo ya Rais kwa Mlipakodi Bora pamoja na maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yatakayofanyika tarehe 1 Julai 2026, hafla inayolenga kutambua mchango wa walipakodi katika maendeleo ya taifa na kuhamasisha.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, akiongoza kikao kati ya Serikali ya Tanzania na Ujumbe wa Benkiy a Dunia uliyoongozwa na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bw. Firas Raad, ambapo walijadili kuhusu miradi ya kipaumbele ya Serikali itakayofadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia Mzunguko wa 21 (IDA-21), kwa lengo la kuharakisha utekelezaji wa agenda ya maendeleo ya Taifa, kilichofanyika ofisi za wizara jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Wizara ya Fedha na Wizara ya Mipango na Uwekezaji, baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitisha kwa kishindo Bajeti Kuu ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2026/27 kwa asilimia 97.66 baada ya wabunge 385 kupiga kura ya ndio kuunga mkono Bajeti hiyo.
Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (EIB) zimekubaliana kuharakisha hatua za kukamilisha mikataba ya ufadhili wa Mradi wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira wa Jiji la Mwanza Awamu ya Pili (LV WATSAN II), unaolenga kuboresha upatikanaji wa huduma za maji safi na usafi wa mazingira kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza na maeneo jirani.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) na Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Balozi Dkt. Bekir Gezer, wakibadilishana Mikataba ya Kuondoa Utozaji wa Kodi Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji wa Kodi katika Mapato (DTA), baada ya kusaini mikataba hiyo katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Hoteli ya Hyatt Regency, jijini Dar es Salaam, ambapo hatua hiyo inatarajiwa kuchochea uwekezaji na biashara kati ya mataifa hayo mawili.
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Natu El-maamry Mwamba na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered, Bw. Herman Kasekende, wakisaini Mkataba wa kugharamia ukamilishaji wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge -SGR), kipande cha tatu (loti 3) na cha nne (loti 4) kutoka Makutupora ya mkoani Singida hadi Isaka, yenye thamani ya takriban dola za Marekani bilioni 1.277, katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kambarage, Treasury Square, jijini Dodoma.