Madhimisho Miaka 50 ya Uhuru, Viwanja Vya Mnazi Mmmoja Kuanzia Tarehe 24-31 Oktoba 2011
Mhe. Paul M. Bomani
1962 - 1965
Mhe. Amir H. Jamal
1966 - 1972, 1976 - 1977, 1982
Mhe. Cleopa D. Msuya
1974 - 1975, 1986 - 1989
Mhe. Edwin Mtei
1978 - 1981
Prof. Kighoma A. Malima
1983 - 1985, 1993 - 1994
Mhe. Steven A. Kibona
1990 - 1993
Mhe. Jakaya M. Kikwete
1994 - 1995
Prof. Simon M. Mbilinyi
1995 - 1996
Mhe. Daniel N. Yona
1997 - 2000
Mhe. Basil P. Mramba
2001 - 2005
Mhe. Zakia H. Meghji
2005 - 2007
Mhe. Mustapha Haidi Mkulo
2008 - Mpaka sasa
Mishahara
Maboresho katika Malipo ya Mishahara
SACCOS
Sir.Ernest Vassey
Waziri wa Fedha wa Kwanza.
Tovuti Maalum ya Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 50 - Wizara ya Fedha
Historia Fupi ya Wizara ya Fedha
Wizara ya Fedha ni moja kati ya Wizara zilizoanzishwa mara baada ya kupata Uhuru mwaka 1961. Serikali ya Kwanza iliyoundwa baada ya kupata Uhuru ilianza kutekeleza majukumu yake mwaka 1962, ambapo Hati ya Majukumu ya kila Wizara ilitolewa na kuanisha wajibu wa kila Wizara.
Wizara ya Fedha ilipitia mabadiliko mbalimbali ya Uongozi lengo likiwa ni kuongeza ufanisi katika usimamiaji wa shughuli za Serikali. Mabadiliko haya yalilenga katika maeneo ya Uongozi, Majukumu na hata jina la Wizara limekuwa likibadilika mara kwa mara ili kukidhi utekelezaji wa mjukumu inayopangiwa.
Kumbukumbu mbalimbali zilizopo zinaonyesha kuwa kwa nyakati tofauti Wizara ya Fedha imekuwa ikiitwa, Wizara ya Fedha(1962), Wizara ya Fedha na Mipango(1976), Wizara ya Nchi, Mipango na Uchumi(1983), Wizara ya Fedha na Uchumi(2008) na Wizara ya Fedha(2011). Mabadiliko haya yalilenga kuongeza ufanisi katika usimamiaji wa shughuli za Serikali.
Kutoka mwaka 1962 ilipoundwa Serikali ya kwanza mara baada ya kupata Uhuru hadi sasa, Wizara ya Fedha imeongozwa na Mawaziri 12 katika vipindi tofautiĀ na Manaibu Waziri zaidi ya 10. Kama ilivyo sasa uteuzi wa Manaibu Waziri ulizingatia uwakilishi kutoka pande zote za Muungano wa nchi yetu.